Monday, May 7, 2012

JITAMBUE

Kila binadamu ana vitu vya kushangaza na vikubwa,karama na utofauti wa pekee.Kwa bahati mbaya watu wengi bado hawajajijua na pia kiasi wanachoweza kufanikisha.Wanaume na Wanawake wamebarikia KARAMA na kujazwa vipawa ambavyo vikitumiwa vinaweza kulisha ulimwengu lakini wamebaki kuwa ombaomba na kuendelea kuwa maskini.
Siku utakayojitambua itakuwa ndio siku yako ya kurejeshwa,siku ambavyo utagundua ulimwengu unavyokuita sivyo,siku hiyo ndio utauga umaskini milele na milele,Mwanafalsafa wa zamani wa Kigiriki aitwaye SOCRATES alisema " MWANADAMU UNAPASWA UJITAMBUE" maneno hayo matatu labda ndiyo yalimwongoza katika falsafa hio kubwa. Kwa nini? Kwa sababu ilikuwa imejaa maana "mwanadamu lazima ujitambue" Mungu aliumba kila nafsi na kuzifungamanisha pamoja na KARAMA ambayo huwawezesha kuishi maisha ya bila kuwa na jasho wala mihangaiko duniani.Inaweza isiaminike lakini ukweli ndio huo.Kama hujijui wewe ni nani na ulichonacho ndani yako,utabaki kuwa mtumwa na kufanya kazi kwa ajili ya ndugu.Wale ambao wamewekeza karama zao na kuzitawala ni waajiri wa kazi,ni viongozi katika maeneo yao na ni mabingwa wa uchumi katika mazingira yao.

Uelewa juu ya hili ndio unaowatofautisha na wengine,kama vile BILL GATES, mtaalamu wa programu za kompyuta,Wengine ni THOMAS A EDSON mgunduzi wa taa ya umeme, ALEXANDER GRAHAM BELL aliyegundua simu,GOOD YEAR aliyegundua na kuzalisha magurudumu ya gari kwa kutumia mipira ya kawaida, OPRAH WINFREY aliyegundua mafanikio yake kupitia kipaji chake cha kuongea,maisha yake yote ni kuongea hufanya mazungumzo ya wazi na hujitengeneza mamia ya dola za kimarekani kwa saa. Ni tajiri na ana uwezo wa kutosha wa kutoa.kuna kitu fulani zaidi yetu,ndani yetu kinachotoa shauku ya kujieleza


Nguvu ya kufanikiwa na kutengeneza pesa imo ndani yetu lazima uitoe mwenyewe,ukiwa au bila elimu ya chuo kikuu nguvu hii ya ndani unaweza kukamilisha chochote kama itaruhusiwa kutekeleza.mheshimiwa bili gates ilimpasa aache shule(pale havard university) pale alipotambua nguvu iliyomo ndani yake.aliacha chuo ili aweze kuiruhusu nguvu iliyomo ndani yake ifanye kazi.Na kwa kweli utele wa pesa isizo na idadi ulimfuata. Ndani ya kila mmoja wetu kuna KARAMA moja ya kipekee, UJASIRI na UMAHIRI usio wa kawaida uwezao kubadilisha ULIMWENGU , KUJITAMBUA kwetu ndiko kunakotutofautisha na wengine washindi na wapotezaji.Watu wengi zaidi ambao wana vipaji vizuri,karama hujikuta wakigandamiza vipaji na karama zao hizo,aidha kwa kutotambua UWEPO WAKE au Kwa kukosa UJASIRI WA KUTHUBUTU. UKIJIGUNDUA WEWE NI NANI NA UKAWA NA UJASIRI WA KUVIELEKEZA KITU HICHO,MAFANIKIO YATAKUFUATA

ahsante kwa kutembelea blog hii,karibu tena.bwana akubariki
wako

mchumi faraja.
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.