Ni rahisi
mtu kukata tamaa pale mambo yanapomuendea vibaya au anapopata ugumu ambao
hakuutegemea hapo awali alipokuwa akipanga mipango yake. Kukata huko tamaa
ndipo panapompelekea mtu kutoweza kufikia makusudio yake. Jambo lolote
lililofanyika na kufanikiwa kasoro mbalimbali zilitatuliwa.
Ni vyema
ukaelewa changamoto zitakuwepo katika kila kitu unachotaka kufanya, kwa
kufahamu hivyo utaweza kufanya mambo yako mpaka yatimie bila kukatishwa na
vikwazo au sababu nyinginezo ikiwemo ''kukata tamaa'' hata pale unapopata
shida.
Wazo la
kukata tamaa ni adui wa wewe kutofanikisha ulichokianza, hivyo nimeona niandike
sababu tano(5) za wewe kutokata tamaa zikusaidie kushikamana na malengo yako.
1. Kukata tamaa hukufanya ufikie kikomo cha
mafanikio.
-Moja ya
sababu ya watu wengi kushindwa kufanikiwa katika mambo yao ni kukata tamaa
mapema kabla hajafika mbali kuendelea kufanya alichokianza. Kukata tamaa ni
kudhihirisha hutaki tena kufanikiwa kwa maana ya hutofanya chochote kuhusiana
na hicho ulichoamua kuacha. Kuwa mstahimilivu na ushikamane na malengo yako
mpaka mwisho.
2. Kukata
tamaa ni kuamua umepoteza muda wako wa thamani.
-Unaweza
kuwa umetumia nguvu na muda wako mwingi kufanya kitu fulani ambapo thamani yake
ni kubwa ya kuweza kukugarimu iwapo utaachana na malengo yako kwa kukata tamaa.
Mfano mzuri ni ‘’usiku wenye giza na mchana wenye mwanga’’ linapoingia giza leo
jioni kesho yake hakuwezi pambazuka mpaka upite wakati wa giza nene usiku wa
manane ndio mwangaza utokee wakati wa asubuhi. Kwa mfano huo halisi ni kwamba
unapokata tamaa wakati huko nyuma umejitahidi kwa kadri uwezavyo ni sawa na
kuishia njiani ukiwa umeshafika karibu kabisa na mahali ulipotaka kufika.
3. Kukata
tamaa ni dhana mbaya ya kujiona umeshindwa.
-Huna sababu
ya kukata tamaa ikiwa wengine wameweza. Ikiwa unataka kufanikiwa muda mzuri wa
kujipa matumaini kuwa unaweza ni pale unapojihisi unataka kukata tamaa.
Usikubali hisia zako zinazokusukuma ukate tamaa zikutawale. Lady Jay Dee, Asha
Rose Migiro au Ali Remtulla wasingeweza kuwa na mafanikio makubwa ya kazi zao
kama wangekata tamaa na mambo wanayofanya. Unaposhindwa kitu jaribu tena na
tena bila kukata tamaa na hii ndio siri
ya kutumiza malengo yako.
4. Kukata
tamaa ni kikwazo kidogo kinachokuzuia kufanya mambo makubwa.
-Mambo yote
mazuri tunayoona leo yamehangaikiwa kwa kutengenezwa na kuwa kama yalivyo.
Amani na uhuru tulio nao leo wazee wetu na watu mbalimbali walipigania mpaka
kufikia sasa. Huwezi jua uwezo wako ni mkubwa kwa kiasi gani mpaka uthubutu
kutenda makubwa licha ya kuwa utakumbana na vikwazo. Kutokata tamaa kwako ndiko
kutakokuwezesha kufanya mambo makubwa na kukufanya uwe mtu bora uliyekomaa.
5. Kukata
tamaa ni kizuizi cha kufikiri njia mbadala ya kuendelea kuyaendea malengo yako.
-Matatizo
mengi yanaufumbuzi ikiwa tutafikiri vizuri, kukata tamaa ni sawa na kusema
hakuna njia nyingine yeyote ya kutatua shida yako. Kizuizi hiki cha kukata
tamaa kinaweza kukufanya ushindwe kufikia malengo yako kwasababu tu
yakupungukiwa na mawazo sahihi yakukuwezesha utafute njia mbadala na kuendelea
kuyaendea na malengo yako.
CREDIT SAIDI KAMOTA