Monday, February 24, 2014

UPO KUNDI GANI KATIKA HAYA?


leo ngoja nizungumzie makundi matatu ya watu duniani halafu utajiangalia uko kundi gani halafu utachukua maamuzi kuwa katika kundi lipi?i
1.SURRENDER COMPLETELY(Wameshakata tamaa kabisa)
Kundi hili ni kundi kubwa sana dunia ya leo,hawa wamebakia wakisema hatuna bahati katika maisha haya na hawajihangaishi tena.Huenda wamewahi fanya vitu kwaajili ya kuinua maisha yao lkn kwa kuwa maisha yanahitaji roho ngumu na kujituma walifeli na sasa wameshakata tamaa.Hawa ukiwaambia fanya kitu flani atakwambia mimi siwezi nitapoteza muda tu.Mwisho wa siku huwa wanakufa masikini kabisa.

2.SURRENDER PARTIALLY(Hawa hawajaka tamaa kabisa lkn hawajiamini)
Kundi hili la watu huwa hawajiamini kabisa kwa kila wanachofanya,unaweza kumwambia fanya kitu kitu flani unaweza inua maisha yako,huenda akakwambia subiri kidogo najipanga bado sio kwamba uwezo hana lkn bado hajiamini,wengi wao wanapotaka kufanya kitu,huhitaji kwenda kwa marafiki zao kwa ushauri,eti shost unaionaje hii,mwingine jamaa unaionaje hii yeye kashindwa unafikiri atakupa jibu gani? atakwambia huwezi.lkn pia hawa unaweza mwambia kufanya kitu kwa ajili ya maisha yake akafanya lkn akafanya anasema ngoja nibahatishe tu.Hawa huwa wanafanya kazi moja miaka miingi lkn huwa hawapigi hatua yoyote..

3.SURVIVORS AND WINNERS(Wasio kata tamaa na washindi)

Kundi hili huwa ni la watu wachache saana huitwa RISK TAKER(FIGHTERS).Watu hawa huwa hawajali, wako tayari kufanya chochote cha halali ili kuhakikisha wanaishi maisha bora au kuongeza kipato,kundi hili huwa hawaridhiki na mwanya mmoja wa kipato ukimwambia leo kuna kitu unaweza fanya na ukaongeza pesa huwa haraka sana kukusikiliza,na hata kama hana cha kufanya anawaza mambo makubwa na anafikiria kufanya mambo makubwa duniani.
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.