Habari za leo mfuatiliaji wa blog hii
,natumaini wewe ni mzima wa afya njema,leo nilitaka kuongelea nini
kinasababisha tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa, kama hujafanikiwa
au hujafikia malengo yako na unayataka kufikia malengo yako basi ni vizuri
kujifunza kwa wale ambao wamefanikiwa ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika,
kwa utafaiti uliofanywa na chuo kikuu cha Havard kwa baadhi ya watu
waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa wana tabia zilizofanana na hio ndio sababu
kubwa inayowaotafautisha na wale wasiofanikiwa, kwa hiyo kwasisi ambao tupo
katika mapigano ya kutaka kufanikiwa ni vizuri kujifunza tabia za wale
waliofanikiwa ,ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika. Hizi ni baadhi ya sifa
ambazo watu wamefanikiwa wanazo,
1. LENGO KUU KWENYE MAISHA
Wengi waliofanikiwa maishani wana
malengo waliojiwekea ili kufanikisha ndoto zao walizonazo maishani.
Umihimu wa lengo
-Ufanisi
-kujua wapi unakwenda na nini
umefanikisha
-kuwekeza nguvu zako zote kufanikisha
hilo lengo.
2. MUDA
Watu waliofanikiwa hakuna jambo
wanalolipa kipaumbele kama muda,ni namna gani wanatumia muda wao vizuri,hawana
muda wa kupoteza,anajua afanye nini na kwa wakati gani,wakati wote yupo ndani
ya muda, pia analotakiwa kufanya leo basi analifanya leo. Kuna kanuni mbili
katika kutumia muda vizuri
1. KANUNI YA PARETO ( 80/20)
-Asilimia 80 ya mafanikio yako
yanatokana na asilimia 20 ya muda wako na jitihada
80% of your success comes from the
result of 20% of your time and effort.Katika kanuni hii ukiutumia muda wako na jitihada vizuri katika yale mambo ya msingi au muhimu tu basi asilimia 20 tu ya muda wako na jitihada inaweza kuchangia mafanikio yako asilimia 80.Hebu piga hesabu kwa siku unatumia muda kiasi gani kwenye mitandao ya kijamii? (Facebook+Whatsapp+Instagram+Twiter+Bbm+Viber+Badoo+Tango N.K) sasa hebu chukua nusu tu ya muda unaotumia katika mitandao ya kijamii ,ukawekeza huo muda kwenye mambo ya maana katika muda wa miezi sita utakuwa wapi? Watu waliofanikiwa hutumia kanuni hii ya PARETO vizuri na kupata mafanikio.
2.PARKNSON LAW
“Work expands to fill the time
available for its completion.”
-Kazi inachukua muda mrefu kutokana
na muda uliweka kufanya kazi hio,ukiweka masaa nane kufanya kazi Fulani basi
itakuchukua masaa nane kufanya kazi hio lakini kazi hiyo hiyo ukijipa masaa sita
pia utaifanya ndani ya masaa sita kama ulivyopanga. Hizi ni kanuni mbili kama
utaziunganisha kwa pamoja basi zitakupa matokeo mawili makubwa
1.Utafanya yale mambo ya msingi tu
unayotakiwa kufanya
2.Utatumia muda mdogo katika kila
unachokifanya.
3. KUJIAMINI
Watu wengi waliofanikiwa na kufanya
mambo makubwa maishani wanajiamini, wanajiamini wao wenyewe na kwa kile
wanachokifanya,wanajiamini katika kuchukua hatua, ili ujiamini zaidi unatakiwa
ufanye mambo mawili
• Kukumbuka
yale mazuri yote ya nyuma uliyoyafanya kwa usahihi
• Kushinda
hofu ya kushindwa,mara nyingi sana watu wasiojiamini hushindw hata kabla ya
kuanza jambo, kisa kuogopa watashindwa