Thursday, April 24, 2014

TABIA KUMI ZINAZOFANANA ZA WATU WALIOFANIKIWA ZAIDI MAISHANI NA KUFANYA MAMBO MAKUBWA


Habari za leo mfuatiliaji wa blog hii ,natumaini wewe ni mzima wa afya njema,leo nilitaka kuongelea nini kinasababisha tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa, kama hujafanikiwa au hujafikia malengo yako na unayataka kufikia malengo yako basi ni vizuri kujifunza kwa wale ambao wamefanikiwa ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika, kwa utafaiti uliofanywa na chuo kikuu cha Havard kwa baadhi ya watu waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa wana tabia zilizofanana na hio ndio sababu kubwa inayowaotafautisha na wale wasiofanikiwa, kwa hiyo kwasisi ambao tupo katika mapigano ya kutaka kufanikiwa ni vizuri kujifunza tabia za wale waliofanikiwa ,ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika. Hizi ni baadhi ya sifa ambazo watu wamefanikiwa wanazo,
1.        LENGO KUU KWENYE MAISHA
Wengi waliofanikiwa maishani wana malengo waliojiwekea ili kufanikisha ndoto zao walizonazo maishani.
Umihimu wa lengo
-Ufanisi
-kujua wapi unakwenda na nini umefanikisha
-kuwekeza nguvu zako zote kufanikisha hilo lengo.
2.        MUDA
Watu waliofanikiwa hakuna jambo wanalolipa kipaumbele kama muda,ni namna gani wanatumia muda wao vizuri,hawana muda wa kupoteza,anajua afanye nini na kwa wakati gani,wakati wote yupo ndani ya muda, pia analotakiwa kufanya leo basi analifanya leo. Kuna kanuni mbili katika kutumia muda vizuri
1. KANUNI YA PARETO ( 80/20)
-Asilimia 80 ya mafanikio yako yanatokana na asilimia 20 ya muda wako na jitihada
80% of your success comes from the result of 20% of your time and effort.Katika kanuni hii ukiutumia muda wako na jitihada vizuri katika yale mambo ya msingi au muhimu tu basi asilimia 20 tu ya muda wako na jitihada inaweza kuchangia mafanikio yako asilimia 80.Hebu piga hesabu kwa siku unatumia muda kiasi gani kwenye mitandao ya kijamii? (Facebook+Whatsapp+Instagram+Twiter+Bbm+Viber+Badoo+Tango N.K) sasa hebu chukua nusu tu ya muda unaotumia katika mitandao ya kijamii ,ukawekeza huo muda kwenye mambo ya maana katika muda wa miezi sita utakuwa wapi? Watu waliofanikiwa hutumia kanuni hii ya PARETO vizuri na kupata mafanikio.
2.PARKNSON LAW
“Work expands to fill the time available for its completion.”
-Kazi inachukua muda mrefu kutokana na muda uliweka kufanya kazi hio,ukiweka masaa nane kufanya kazi Fulani basi itakuchukua masaa nane kufanya kazi hio lakini kazi hiyo hiyo ukijipa masaa sita pia utaifanya ndani ya masaa sita kama ulivyopanga. Hizi ni kanuni mbili kama utaziunganisha kwa pamoja basi zitakupa matokeo mawili makubwa
1.Utafanya yale mambo ya msingi tu unayotakiwa kufanya
2.Utatumia muda mdogo katika kila unachokifanya.

3.        KUJIAMINI
Watu wengi waliofanikiwa na kufanya mambo makubwa maishani wanajiamini, wanajiamini wao wenyewe na kwa kile wanachokifanya,wanajiamini katika kuchukua hatua, ili ujiamini zaidi unatakiwa ufanye mambo mawili
•          Kukumbuka yale mazuri yote ya nyuma uliyoyafanya kwa usahihi
•          Kushinda hofu ya kushindwa,mara nyingi sana watu wasiojiamini hushindw hata kabla ya kuanza jambo, kisa kuogopa watashindwa




Share:

SIRI YA KUISHI MAISHA MAREFU



WATAFITIi wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai

Aghalabu maisha ya mwanadamu yeyote yule yapo mikononi mwa muumba wake, ambaye hujua lini muda wa kuishi wa kiumbe wake utakwisha. Lakini mtindo wa maisha yetu usiojali kanuni za afya, umeonyesha kuwa ndicho chanzo cha watu wengi kuishi maisha mafupi.

Kiwango cha maisha ya binadamu sasa kinapunguzwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, mtindo wa maisha na mazingira, lakini wanasayansi na wataalamu wa afya wamekuja na mbinu ambazo zinatajwa kusaidia kuongeza miaka yako ya kuishi.

KUNYWA CHAI
 Watafiti wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai.

Chai, hasa ya kijani (green tea) ina ondoa sumu iitwayo ‘polyphenols’ ambayo husaidia mwili wako kupambana na magonjwa ya moyo. Wataalamu hao wanasema, chai iliyochemka vizuri au pakiti ya majani ya chai kukorogwa vyema katika majimoto, yafaa zaidi. Kwa kifupi, chai ikolee majani.

KUSIMAMA KWA MGUU MMOJA KILA ASUBUHI
 Inaweza kuonekana kuwa ni jambo la ajabu, lakini wanasayansi wamebaini kuwa kusimama kwa mguu mmoja asubuhi kunasaidia kuimarisha misuli ya mgongo, nyonga na tumbo na kuupa uwiano uti wa mgongo.


Mtaalamu wa viungo anasema, zoezi hili jepesi likifanywa kila siku, linatoa manufaa ya muda mrefu na linakukinga kuvunjika mifupa kwa urahisi hasa unapoanza kuzeeka. Tafuta marafiki sita unaowaamini Kuwa na marafiki wazuri na familia ambayo unaiamini ni siri moja kubwa ya kuishi miaka 100.

Utafiti uliofanywa na kitengo cha Maisha na Mazingira katika Chuo Kikuu cha Australia, ulionyesha kuwa kupata watu wa kukupa msaada na kukufariji wakati wa huzuni kunasaidia kuongeza umri wa kuishi kwa kuzalisha kemikali ya ‘furaha’ inayofahamika kama dopamine na oxtocyin ambavyo huusaidia ubongo.

Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu cha Dodoma, anasema unapokuwa na tatizo, kisha ukalihifadhi moyoni, unaunda uchungu ambao unakuathiri. Anasema, mwili wa mtu unaathiriwa kutokana na tabia au matendo ya moyoni, unapohifadhi tatizo bila kupata ushauri unakuza tatizo hilo.

“Marafiki au hata ndugu wa kumweleza tatizo lako ni muhimu, wanaweza kukupoza,” anasema

USISHIBE SANA  
Wakazi wa kisiwa cha Okinawa, nchini Japan, wanaongoza kwa kuwa na kiasi kidogo cha watu wenye unene uliopitiliza (obesity) na wanasifika kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi zaidi ya miaka 100. Siri yao kubwa ni kuwa hawali wakashiba kwa zaidi ya asilimia 80.

Watafiti wa Marekani pia, wamebaini kuwa, binadamu wanaweza kuishi miaka mingi zaidi iwapo chakula wanachokula kinapunguzwa kwa robo tatu. Ina maana kwamba kula kidogo kunaufanya mwili wako usiwe na kazi kubwa ya kumeng’enya, hivyo kuupa nafasi ya kuwajibika na kazi nyingine.

Mtaalamu wa chakula na lishe, anasema, mtu hatakiwi kula akashiba bali anatakiwa aache njaa kwa mbali ili kutoa nafasi ya maji na mmengenyo kuchukua nafasi.
Share:

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.