Wednesday, February 26, 2014

MASWALI 20 MUHIMU YA KUJIULIZA KABLA YA KUANZA BIASHARA




Habari za leo msomaji wa FARAJA MMASA BLOG,natumaini umzima wa afya njema mungu anaendelea kukupigania.leo naandika kuhusu mambo muhimu  ya kujiuliza kabla ya kuanza biashara,wengi wetu tumekuwa tukianza biashara kwa kukurupuka bila kwanza kufanya utafiti wa biashara tunayotaka kufanya na kupata taarifa za kutosha,matokeo yake tunajikuta katika wakati mbaya ,kabla hujafanya au wakati unafanya utafiti wa biashara unayotaka uifanya hebu jiulize maswali haya kwanza


1.         Kwanini nataka kuanza biashara?
2.         Ni aina gani ya biashara ninayoitaka?
3.         Wateja wangu watakuwa wa aina gani?
4.         Nitauza bidhaa au hudama ya aina gani?
5.         Tayari nimejiandaa kutumia muda wangu na pesa kufanya biashara ianze?

6.         Biashara yangu itakuwa sehemu gani?
7.         Watakaokuwa wananiuzia malighafi ni kina nani au bidhaa nitakuwa nanua wapi ?
8.         Ninahitaji wafanyakazi wangapi?
9.         Ninahitaji pesa kiasi gani ili niweze kuanzisha biashara yangu?
10.       Je ninahitaji mkopo?
11.       Itanichukua muda gani mpaka niweze kuanza biashara yangu?
12.       Ninahitaji mkopo?
13.       Itanichukua muda gani mpaka kuanza kutengeneza faida inayoridhisha?
14.       Nani ni washindani wangu wakubwa?
15.       Bei ya bidhaa au huduma yangu itakuwa vipi kulinganisha na washindani wangu?
16.       Nitauweka vipi mfumo wa kisheria wa biashara yangu?
17.       Nitalipa kodi kwa kiwango gani?
18.       Ninahitaji bima ya aina gani?
19.       Nitaingoza vipi biashara yangu?
20.       Je nitaitangaza vipi biashara yangu kuweza kujulikana kwa watu?

Haya ni baadhi maswali ya muhimu ya kujiuliza kabla ya kuanza biashara yako,na haya maswali ndio yatakupa mwanga zaidi wakati unafanya utafiti wa biashara yako,ila nakupa onyo asije mtu hata siku moja akakuambia biashara Fulani inalipa ,na wewe ukaanza biashara kabla hujafanya utafiti wa kutosha kisa tu una hio pesa ya kuanzia biashara.Na katika swali la kumi na mbili nakushauri mara nyingi usichukue mkopo kuanzia biashara bali chukua mkopo kuendelezea biashara yako pale unapoona biashara yako imeimalika.Haya maswali unajiuliza hakikisha unayapatia majibu,siku nyingine nitakuja kuelezea majibu sahihi ya haya maswali ,lakini naamini wewe pia yapo ndani ya uwezo wako kama kweli umedhamiria kuanza biashara
 .
WAKO FARAJA MMASA (MOA)

*SELF -FULFILLING PROPHECY*


************Tafuta mafanikio kama utaishi milele lakini kumbuka kumcha mungu wako na kutenda mema kama leo ndio siku yako ya mwisho kuwepo katika dunia hii*****************************
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.