Sunday, July 21, 2013

MADHARA YAKULAZIMISHA KUKUBALIKA KWA WATU.


Karibu katika Faraja Mmasa Blog,ninatumaini ni mzima wa afya njema.Leo napenda kuongelea mada ya Madhara ya kulazimisha kukubalika katika jamii,nianze kwa kukusimulia kisa kimoja cha SIMBA.
Kulikuwa na simba mmoja alikuwa akiishi katika msitu mkubwa mno na simba wenzie,siku moja simba aliamua kutembea sehemu ambayo walikuwa wakiishi wanyama wengine wanaitwa(HEDHEHOG),baada ya kufika aliipenda sana ile sehemu waliokuwa wakiishi wale wanyama (Hedgehog),akaamua kwenda kwa kiongozi wa wale wanyama(hedgehog's) na akaumilza kama anaweza kuishi eneo lile, Yule kiongozi akamwamba “samahani upo tofauti sana  na sisi,labda uende ukate mkia wako unaweza kufanana nasisi hapo unaweza kuishi na sisi,simba akaondoka akarudi alipokuwa anaishi ,  na akaamua kuukata mkia wake ili afanane na wale wanyama (hedgehog's). Baada ya kuukata akaamua kurudi kwa Yule kiongozi na kumuonyesha namna alivyobadilika,,baada ya Yule kiongozi wa wale wanyama kumuona  akamjibu “lakini mbona bado unaonekana tofauti sana na sisi,labda uende ukaonyoe nywele zako zote labda hapo unaweza kufanana na sisi hapo unaweza kuishi na sisi.

HEDGEHOG

Simba aliona sasa hilo jambo linakuwa gumu sana kwake,lakini kwa kuwa alitaka KUKUBALIKA KATIKA JAMIII YA HEDGEHOG alikuwa hana jinsi akaamua kunyoa nywele zake zote kwa sababu alikuwa na nia sana ya kukubalika na wale wanyama,baada ya kunyoa nywele zake zote akarudi tena kwa Yule kiongozi na kumuonyesha,baada ya Yule kiongozi kumuuona akamwambia “ mmmh unatakiwa kukata kucha zako zote ni ndefu mno hapo utakuwa umefanana na sisi” simba hakuwa na jinsi kwa kuwa alidhamiria KUKUBALIKA ili aweze kuishi katiaka enneo lile akaamua kukata kucha zake zote,baada ya kurudi kwa Yule kiongozi,Yule kiongozi baada ya kumuona akamwamba “ samahani sana pamoja na mabadilko yote uliyoyafanya na utakayoyafanya mi naona HUTAFANANA na sisi kwa sababu hujaumbwa kuwa hedgehog,samahani nakuomba uondoke haraka.
Simba akaondoka huku akijisikia vibaya mno,baada ya kurudi nyumbani kwao akakutana na  kundi la simba likimsubiri ,simba wenzie walikuwa hawajakubali muonekane wake mpya baada ya kujifanyia mbadiliko,simba wenzie wakwambia “wewe sio simba tena,umepoteza KITAMBULISHO CHAKO  sisi hatuwezi kuishi na wewe tena.”
Yule simba akaondoka bila kujua anakwenda wapi na kuanza maisha wapi na kina nani?,alisikitika sana kuondoa uthamani wake  ili aweze kukubalika katika ile jamii ya wale wanyama wa hedgehog na akaambulia patupu.
Kutokana na hio story tunaweza kujifunza mambo mengi katika maisha yetu ya kila siku,wengi wetu tumekuwa tunabadilisha uhalisa wetu ili tuweze kukubalika na baadhi ya watu ,tunabadilisha namna ya uvaaji wetu ili tufanane na wengine mwishowe tunaonekana vituko,tunaacha kuvipenda vile tulivyokuwa tunavipenda mwanzo na kupenda vile vinavyopendwa  na wengine, na matokeo yake tunapoteza ule uthamani wetu tuliokuwa nao,na mwishoni tunanapoteza hata furaha ya maisha tuliyokuwa nayo,tunapoteza KUJIAMIANI kwa sababu tunaishi maisha ya kuigiza,baadae tunatakataliwa na tunapoteza ule utambulisho wetu tuliokuwa nao,kama wadada ambao wanaaharibu ngozi zao ili waonekane tofauti  baadae wanakuja kujikuta kwenye matatizo
 .
Hata kwenye swala la uhusiano wengi wetu tumekuwa mwanzoni tukificha uhalisia wetu ili tupendwe ,tunaficha tabia zetu,tunaficha hali ya maisha kiuchumi tuliyonayo ili tu tuwapate wale tunaowapenda lakini mwishoni huu uigizaji wa tabia hugeuka MWIBA mchungu  katika ndoa zetu na tunakuta tuanshindwa kutoka tena  badala yake maisha yeu yanakuwa na maumivu yasiyokuwa na mwisho ,na furaha maishani mwetu inapotea kabisa.

Ushauri wangu naomba ishi kama wewe,jikubali jinsi ulivyo,kuwa na mfumo wako wa maisha,usiigize maisha ili uuonekane mtu tofauti au kwa kutaka umaarufu,ishi wewe kama wewe,hii itakusadi na kufanya ujiamini na uishi maisha ya furaha na kutambulika kwa watu kutokana na mfumo wako wa maisha ulionao,utakuwa ni UTAMBULISHO WAKO.

Ahsante kwa kutembelea blog hii 
wako faraja mmasa a.k.a moa
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.