Thursday, April 24, 2014

TABIA KUMI ZINAZOFANANA ZA WATU WALIOFANIKIWA ZAIDI MAISHANI NA KUFANYA MAMBO MAKUBWA


Habari za leo mfuatiliaji wa blog hii ,natumaini wewe ni mzima wa afya njema,leo nilitaka kuongelea nini kinasababisha tofauti kubwa kati ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa, kama hujafanikiwa au hujafikia malengo yako na unayataka kufikia malengo yako basi ni vizuri kujifunza kwa wale ambao wamefanikiwa ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika, kwa utafaiti uliofanywa na chuo kikuu cha Havard kwa baadhi ya watu waliofanikiwa kwa kiasi kikubwa wana tabia zilizofanana na hio ndio sababu kubwa inayowaotafautisha na wale wasiofanikiwa, kwa hiyo kwasisi ambao tupo katika mapigano ya kutaka kufanikiwa ni vizuri kujifunza tabia za wale waliofanikiwa ,ili tuweze kufika pale tunapotaka kufika. Hizi ni baadhi ya sifa ambazo watu wamefanikiwa wanazo,
1.        LENGO KUU KWENYE MAISHA
Wengi waliofanikiwa maishani wana malengo waliojiwekea ili kufanikisha ndoto zao walizonazo maishani.
Umihimu wa lengo
-Ufanisi
-kujua wapi unakwenda na nini umefanikisha
-kuwekeza nguvu zako zote kufanikisha hilo lengo.
2.        MUDA
Watu waliofanikiwa hakuna jambo wanalolipa kipaumbele kama muda,ni namna gani wanatumia muda wao vizuri,hawana muda wa kupoteza,anajua afanye nini na kwa wakati gani,wakati wote yupo ndani ya muda, pia analotakiwa kufanya leo basi analifanya leo. Kuna kanuni mbili katika kutumia muda vizuri
1. KANUNI YA PARETO ( 80/20)
-Asilimia 80 ya mafanikio yako yanatokana na asilimia 20 ya muda wako na jitihada
80% of your success comes from the result of 20% of your time and effort.Katika kanuni hii ukiutumia muda wako na jitihada vizuri katika yale mambo ya msingi au muhimu tu basi asilimia 20 tu ya muda wako na jitihada inaweza kuchangia mafanikio yako asilimia 80.Hebu piga hesabu kwa siku unatumia muda kiasi gani kwenye mitandao ya kijamii? (Facebook+Whatsapp+Instagram+Twiter+Bbm+Viber+Badoo+Tango N.K) sasa hebu chukua nusu tu ya muda unaotumia katika mitandao ya kijamii ,ukawekeza huo muda kwenye mambo ya maana katika muda wa miezi sita utakuwa wapi? Watu waliofanikiwa hutumia kanuni hii ya PARETO vizuri na kupata mafanikio.
2.PARKNSON LAW
“Work expands to fill the time available for its completion.”
-Kazi inachukua muda mrefu kutokana na muda uliweka kufanya kazi hio,ukiweka masaa nane kufanya kazi Fulani basi itakuchukua masaa nane kufanya kazi hio lakini kazi hiyo hiyo ukijipa masaa sita pia utaifanya ndani ya masaa sita kama ulivyopanga. Hizi ni kanuni mbili kama utaziunganisha kwa pamoja basi zitakupa matokeo mawili makubwa
1.Utafanya yale mambo ya msingi tu unayotakiwa kufanya
2.Utatumia muda mdogo katika kila unachokifanya.

3.        KUJIAMINI
Watu wengi waliofanikiwa na kufanya mambo makubwa maishani wanajiamini, wanajiamini wao wenyewe na kwa kile wanachokifanya,wanajiamini katika kuchukua hatua, ili ujiamini zaidi unatakiwa ufanye mambo mawili
•          Kukumbuka yale mazuri yote ya nyuma uliyoyafanya kwa usahihi
•          Kushinda hofu ya kushindwa,mara nyingi sana watu wasiojiamini hushindw hata kabla ya kuanza jambo, kisa kuogopa watashindwa





4.        UTEKELEZAJI ZAIDI KULIKO MANENO (KUWA MTU WA VITENDO)
Watu waliofanikiwa na kufanya mambo makubwa zaidi ni watu wa matendo zaidi kuliko kuongea, ni watu wa ku take action, hivyo basi ili ufanikiwe unahitaji kuwa mtu wa vitendo zaidi na sio wa maneno. Na mara nyingi huwa sio watu wa wakusubiri wakati sahihi kufanya jambo, wao huchukua hatua na kuanza kufanya baada ya kujiridhisha kwa utafiti ,baada ya kupata matokeo ya kile walichokifanya kama kuna mabadiliko yanatakiwa hufanya marekebisho na kusonga mbele. Hivyo hivyo ndugu msomaji
unayesoma kama unataka kusonga mbele aanza kuchukua hatua badala ya maneno mengi, acha kuwa muongeaji wa mipango isiyotekelezeka, nitafanya hichi nitafanya kile muda unazidi kwenda bila kufanya kitu chochote.
5.        NI WATU WA KUTOA MISAADA
Kuna nguvu kubwa zaidi katika utoaji ,na watu waliofanikiwa mara nyingi wanakuwa wamegundua nguvu hii kubwa katika mafanikio yao,ndio maana leo hii unaweza sikia mengi anatoa misaada kila kukicha, katika maisha yetu ya kila siku ili upokee ni lazima utoe kwanza, hata katika maisha yetu ya kila siku ya kawaida tu ,kwa mfano ili uheshimiwe na watu ni lazima kwanza ujiheshimu na uheshimu watu wengine, ili uthaminiwe lazima uthamini kwanza hata kwenye uhusiano ili upendwe lazima na wewe uonyeshe upendo kwanza.Utarejeshewa kile utakachotoa. Ili mungu akubariki ni lazima uwe mtu wa kutoa sana kwa wengine hasa kwa wale wasiojiweza, na hata kama wewe ni maskini lazima unakitu tu cha kusaidia wengine ,kwa mfano kuna habari moja hivi
Siku moja mtu mmoja alimuuliza Buddha,” kwanini mimi ni maskini sana?”
Buddha akamjibu “ kwasababu hujajifunza kutoa”
Yule mtu akamjibu” mimi maskini sina kitu chochote cha kutoa msaada?”
Buddha akamjibu “ unavyo vitu vichache vya kutoa”

Uso: ambao unaweza kumpa mtu tabasamu
Mdomo; kwa ajili ya kuwapa watu maneno ya kuwafariji
Moyo :kuwa mwema kwa watu kwa kuwaonyesha upendo
Macho:kuwaangalia watu kwa uzuri
Mwili:ambao unaweza kuutumia kusaidia wengine

Buddha mwisho akamwambia hakuna mwanadamu aliye maskini kabisa akakosa kuwasaidia wengine “poverty of spirit is the real poverty”.Ndugu msomaji ni mara ngapi unashindwa kuwasaidia wasiojiweza na uwezo unao,jiulize leo toka umetoka asubuhi umekutana na watu wangapi wasiojiweza au walemavu lakini umetoa hata shilingi 200 yako? unanguo ngapi nyumbani zinakubana umeweka kwenye kabati lakini kuna watu kibao unaowafahamu wanahitaj hizo nguo hawana nguo za kuvaa? 
6.        KUJISIOMEA MARA KWA MARA.
Mara nyingi watu waliofanikiwa ni wasomaji wazuri wa mambo mbalimbali ,wanakiu ya kutaka kujua mambo mapya kila siku,kila siku wanahakikisha wanaingia kitu kipya kwenye akili zao,kusoma mambo mbalimbali ikiwemo vitabu, majarida,magazeti.Kusoma vitabu mbalimbali mara nyingi inakuwezesha kupata mawazo mapya kila siku na kukuza ufahamu wako,kila siku huwa ninasema hili ninapokuwa ninafundisha semina,kila siku ni nilazima uhakikishe unakua kimwili ,kiakili,na kiroho .kwa mfano huwezi kuendesha biashara kiufasaha kwa degree yako ya uhandisi ni nilazima ujisomee wewe mwenyewe maswala ya biashara ili uweze kufanya biashara,hata kwenye mahusiano yetu au ndoa zetu ni lazima usome vitabu mbalimbali ili uweze kujua njia ya kuindesha ndoa yako kwa mafanikio,usiishi kwa kuamini hicho hicho kila siku.
7.        KUKUBALI WANAPOKESEA.
Kuna mambo mawili kama unayafanya basi itakuwa ngumu kupata mafanikio.Mambo hayo ni
•          Blaming others,kama kunakitu hakijaanda sawa na wewe ndio umesababisha wewe unakuwa ni mtu wa kulaumu wengine tu na kuona wao ndio waliokosea tu,hapa huwezi kujifunza kitu na kila siku utafanya makosa yale yale,utashanga husongi mbele kumbe ni makosa yako wewe mwenyewe.watu wengi waliofanikiwa hukubali pale walipokosea,hukubali makosa yao na kuyafanyia marekebisho.
•          Making excuses. Hii huwa nasema ni kujihurumia,hukosi sababu hata kama ni kwa ajili ya uzembe lakini utatafuta sababu ili usijione mzembe,sifanya hivi kwasababu ya kitu Fulani kumbe ni uzembe tu ulionao.

8.        NI WATU WANAOBADILIKA KUTOKANA NA MAZINGIRA.
Mara nyingi watu waliofanikiwa ni watu wanaobadilika kutokana na mazingira waliyonayo,hubadilika kutokana na mazingira pia husoma alama za nyakati,hivyo hivyo kama unahitaji kupigia hatua ni lazima ukubali kubadilika usifanye yale yale kila siku,kwa style ile ile,dunia inabadilika.Ni lazima ukubali kubadilika kuendana na hali halisi.Steve jobs alianza na kompyuta ,then animation mwishoni akaibukia kwenye Ipod,ipad n.k
9.        WANANDOTO KUBWA ( BIG DREAMER)
Kitu kingine kinachowataofautisha waliofanikiwa na wasiofanikiwa ni namba wanajiwekea kufanikisha ndoto walizonazo maishani,watu waliofanikiwa zaidi basi huwaza ndoto kubwa na hii huawezesha kutumia nguvu kubwa muda,na mipango inayotekelezeka ila kutimiza ndoto zao.Hata watu wasiofanikiwa nao hufikia malengo yao tatizo kubwa hujiweka ndoto ndogo na kuzifanikisha. Chochote anaoamini mwanadamu huweza kukifanikisha .Ubongo ni kama ardhi yenye rutuba ila inategemea wewe unapanda nini kichwani mwako? Hapo mwanzo watu waliamini watu hawatapaa angani lakini Orvile and Wilbur Wright wakaamini inawezekana .,maandishi hayatumwa hewani na kumfikia mtu Lakini Eng Matti Makkoen aliamini inawezekana na december 1992 Sms ya kwanza ikatumwa kupitia simu kwenye mtandao wa Vodafone Gsm Network wa Uk.Thomas A Edson yeye aliamini na kuwa na ndoto ipo siku kuna taa itatumia umeme badala ya mafuta baada ya miaka zaidi ya kumi ya majaribio na kushindwa zaidi ya mara 999 lakini mara ya 1000  taa ya kutumia umeme ikawaka.na ndio hio unayoiona sasa inawaka chumbani kwako,sebleni au ofisi kwako.
Eng Matti mgunduzi wa kwanza wa kutuma Msg kwa kutumia simu
Wright Brothers wagunduzi wa kwanza wa ndege

Thomas A Edson mgunduzi wa taa inayotumia umeme
10.      TABIA NJEMA NA UAMINIFU.
Hii hufanya kukubalika kwa watu na jamii yote kwa ujumla.Uaminifu ni jambo kubwa zaidi  katika maisha ya mwanadamu ,Watu waliofanikiwa mara nyingi huwa waaminifu na hii huwafanya Watu,Makampuni,Taasisi kuwa na imani nao kufanya Biashara.Basi swala la kuwa Muaminifu ni swala lisilokwepeka pale tunapotaka kupiga hatua kwenye maisha yetu.
AHSANTE  KWA KUTEMBELEA BLOG HII,



WAKO FARAJA MMASA
Wako faraja mmasa a.k.a MOA.
x+3P
* SELF FULFILLING PROPHECY*

************Tafuta mafanikio kama utaishi milele lakini kumbuka kumcha mungu wako na kutenda mema kama leo ndio siku yako ya mwisho kuwepo katika dunia hii*****************************
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.