Monday, August 19, 2013

MBINU 20 KWA MWANAFUZI/MWANACHUO KUPATA MAFANIKIO KWENYE MASOMO YAKE- PART 2



Karibu katika blog ya FARAJA MMASA BLOG,naamini ni mzima wa afya njema,mungu aliyetuumba anaendelea kutupigania kwa namna moja au nyingine,leo naendelea sehemu ya pili (part 2) ya somo la mbinu 20 za mafanikio katika masomo,ni somo zuri kwa wanafunzi na wanchuo ili kuweza kujipatia mafanikio katika masomo yao na maisha yao kwa ujumla,kama hujasoma sehemu ya kwanza basi unaweza kubonyeza hii link Katika somo la leo nitajikita zaidi katika utunzaji wa kumbukumbu,ambalo ni jambo muhimu zaidi kwa mwanafunzi MBINU 2O KWA MWANACHUO/MWANAFUNZI KUPATA MAFANIKIO KWENYE MASOMO-PART 1 ili kuweza kupata mafanikio katika masomo yake.Uchunguzi unaonyesha kuwa watu ambao huzingatia suala la kanuni za afya zikiwemo mbinu za kutunza kumbukumbu ya akili hupunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa seli zinazojenga uwezo wa akili katika kutunza kumbukumbu(suzan tapert mwanasaikolojia kutoka Chuo cha Califonia san Diego nchini Marekani anathibitisha haya pia) ili mwanafunzi aweze kutunza na kujiongezea kumbukumbu zake basi inampasa kuyafanya haya yafuatayo


     6.LISHE BORA
Ni wazi kuwa watu wengi tunafahamu maana ya lishe bora,lakini kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na chuo cha American Acedamy of Neurology kinachojihususha na mambo ya neva ,ulibaini kuwa machungwa,spinachi,karoti,mogamboga,viazi vitamu huuongezea uhai ubongo na kufanya mwanadamu asiweze kushambuliwa na magonjwa ya kupooza.

Aidha matunda na vyakula vyenye vitamini b,folik acid (folic acid) ,niasin (niacin) kalkamin( curcumin) husaidia kufanya ubongo uwe na mawasiliano ya kutosha na viungo vingine vya mwili na kupunguza kwa asilimia 11 uhalibifu wa seli ndani ubongo.Utafiti wan National Reseach Council Nchin Milan,Italy unathibitisha kuwa vyakula vyenye vitamin E hupunguza kiwango cha usahaulifu.

7.MAZOEZI YA MWILI
Ufanyaji wa mazoezi ya mwili huimarisha misuli na kusaidia akili kuweza kufanya kazi vema,hii inatokana na ukweli kwamba tunapofanya mazoezi tunakuwa  tunaongeza msukumo msukumo wa damu mwilini na hivyo kuufanya ubongo kufikiwa na damu ya kutosha ambayo ni muhimu kwa uimara wa kumbukumbu.mara nyingi mazoezi yanayofaa zaidi kwa afya ya mwili na uimarishaji ni yale ya asubuhi na jioni. Kuhusu aina ya mazoezi inategemea na umbo la mtu lakini kukimbia kuruka kamba,kucheza mpira ni bora kwa afya..Mazoezi ya aina hii yakifanywa  na Wanafunzi huwasaidia pia kutunza utunzaji wa kumbukumbu  za masomo wanayofundishwa.


 8.UTUMIAJI WA VINYWAJI

Vinywaji kama kahawa,chai nyeusi navyo huchangia kuongeza uwezo wa ubongo kutunza kumbukumbu,inashauriwa kwa mwanadamu kutumia walau  kikombe kimoja cha vinywaji hivyo ili kuongeza enzymes ambazo ni muhimu  kwa kuongeza nguvu ubongo ili kuweza kutunza kumbukumbu,hata hivyo vinywaji vikali kama pombe havirusiwi  kwani huchangia kudumaza uwezo wa kumbukumbu.
Baada ya kuangalia mambo muhimu katika utunzaji wa kumbukumbu,basi tuendelee na mbinu nyingine ambazo pia ni muhimu ili uweze kupata mafanikio katika masomo yako

9.UNAPOKUWA DARASANI MSIKILIZE MWALIMU KWA UMAKINI MKUBWA
Wanafunzi wengi wanapokuwa darasani hasa katika hichi kizazi cha mtandao wanakosa umakini katika kumsikiliza mwalimu ,pale anapokuwa anafundisha.Hakikisha mwalimu anapokuwa anafundisha unaweza kumsikiliza kwa umakini huku ukiwa na NOTEBOOK ili kuweza kuandika vile vitu muhimu ambavyo vitakuwa na msaada katika siku za mbeleni,hakisha pale unaposhindwa kuelewa unanyoosha mkono na kumuuliza mwalimu kwa kile usichoelewa ingawa katika shule zenu nyingi hasa za kayumba utaonekana unajishaua sana,ndugu yangu angalia nini unahitaji na sio watu watasema nini juu yako shuleni ulienda peke yako na ipo siku utaondoka peke yako,hakikisha unaondoka na ulichofuata. Swala la msingi hapa unapokuwa darasani kufunga ubungo wako katika maswala yote na kubaki kumsikiliza mwalimu tu,kama ni mwanachuo zima simu yako au weka silent kwenye begi mpaka utakapotoka  ili usiweze kuhamisha akili yako sehemu nyingine kwa mfano pale itakapoingia mesegi,hakikisha kila kipindi kikiisha umeingiza kitu kipya ambacho ulikuwa hukijui hapo kabla.
10.JIANDAE KWA KILA KITU KABLA HUJAANZA KUJISOMEA BINAFSI
Ni lazima kwa kila mwanafunzi kuwa na muda maalam wa kujisomea yeye mwenyewe binafsi ukiacha na ule muda wa jadiliana katika makundi mbalimbali,hakikisha kabla hujaanza kusoma umeandaa kila kitu cha msingi unachotakiwa kuwa nacho ,kama unasoma hesabu basi hakikisha vitu vyote vinavyohusiana na somo la hisabati,kama  ni calculator,penseli,mkebe ,past papers,vitabu ,sio unasoma mara umesahau kitu kipo kwa rafiki yako kwa hiyo ufunge tena safari,au umeshau chumbani,hii itakufanya ukose utulivu ,jua kabisa leo nina ratiba ya somo Fulani kwa hiyo fanya maandaliza toka mapema,pia hakikisha unasaa pembeni ili ujue kabisa muda unaotumia katika kusoma,kama ni masaa mawili basi ujue ni masaa mawili,maana unaweza kuwa umetumia nusu saa tu ndio uliyotulia na kusoma muda wote ulitumia katika kutembea tembea
Usikose sehemu ya tatu ya mada hii hapa
Wako faraja mmasa a.k.a moa
Kama hujasoma sehemu ya kwanza ya mada hii bonyeza hii link hapa
MBINU 20 KWA MWANAFUNZI?MWANACHUO KUPATA MAFANIKIO KWENYE MASOMO-PART 1
Pia nakuomba usikose kusoma kitabu changu kiatakapotoka ambacho kitakufanya upate uelewa wa mambo mengi

***************DUNIANI TUNAPITA USIACHE KUTENDA MEMA,JUA IPO SIKU UTAIACHA HII DUNIA,WAKTI MWINGINE KABLA HUJALA JIULIZE KAMA KESHO HUTAIONA UTAIWEKA WAPI ROHO YAKO BAADA YA MAISHA YA KIDUNIA***************************************
Share:

1 comment:

  1. dawa za nguvu za kiume,,ugumba ,,uti,,,biashara na uchawi,,majini,,kukuza uume,,kuondoa maji mengi ukeni,,,na uzazi wasiliana na dr wa mitishamba 0764839091 tanga

    ReplyDelete

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.