Monday, August 19, 2013

MOURINHO AANZA VYEMA LIGI KUU ENGLAND...CHELSEA YAUA 2-0



KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesherehekea kurejea kwake Stamford Bridge kwa kuanza na ushindi wa mabao 2-0 katika Ligi Kuu ya England dhidi ya timu iliyopanda daraja msimu huu, Hull.
Kiasi cha miaka sita tangu aachane The Blues, kocha huyo maarufu kama Special One alifurahia mapokenzi mazuri na mchezo mzuri wa timu yake akirejea nyumbani.
Haikuwa kazi rahisi kwa Chelsea kushinda, baada ya mkwaju wa penalti wa Frank Lampard dakika ya sita kuokolewa na Allan McGregor na sheria ya teknolojia kwenye mstari wa goli ikachukua nafasi yake wakati kipa huyo wa Scotland alipookoa mpira wa kichwa wa Branislav Ivanovic na kudhaniwa ni bao dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza, ikisahihisha si bao.
Pamoja na hayo, Chelsea ilipata mabao yake yote kipindi cha kwanza kupitia kwa Oscar dakika ya 13 na Lampard dakika ya 25.
Kikosi cha Chelsea leo kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Lampard, Ramires, De Bruyne/Schurrle dk67, Oscar/van Ginkel dk85, Hazard, Torres na Lukaku dk75.
Hull City: McGregor, Elmohamady, Chester, Davies, Figueroa, Brady, Meyler/Huddlestone dk59, Koren, Sagbo, Graham/Livermore dk59 na Aluko/Boyd dk79.

He's back: Jose Mourinho blows kisses to the Stamford Bridge crowd on his return
Amerudi: Jose Mourinho akiuonyesha ishara ya busu umati Uwanja wa Stamford Bridge katika kurejea kwake
Comfortable: Oscar set Chelsea going in the 13th minute and there was no way back for Hull from there
Shwari kabisa: Oscar akishangilia na Torres baada ya kufunga
Easy does it: Oscar celebrates scoring the opening goal
Rahisi namna hii: Oscar akishangilia
Caught in two minds: Allan McGregor tried to punch a bouncing ball and caught Fernando Torres instead
Allan McGregor akijaribu kupangua dhidi ya Fernando Torres
Missed: Frank Lampard saw his penalty saved by McGregor
Anakosa: Frank Lampard alishuhudia mkwaju wake wa penalti ukiokolewa na McGregor
Not to be deterred: Lampard thundered in a free kick shortly after the penalty miss
Anasahihisha makosa: Lampard alisahihisha makosa yake kwa kufunga kwa mpira wa adhabu muda mfupi baada ya kukosa penalti
Lampard
Seven passes and in: Chelsea moved quickly to pull Hull apart before Oscar scored
Pasi saba: Chelsea ilifanya shambulizi la haraka kuibomoa ngome ya Hull kabla ya Oscar kufunga
Stopped: McGregor parried away Branislav Ivanovic's header
Amezuia: McGregor akizuia mpira wa kichwa wa Branislav Ivanovic
No goal: GDS said Branislav Ivanovic's header didn't cross the line
Si bao: GDS imesema mpira wa Ivanovic haukuvuka mstari
Joyous: Fans took to their craft sets again but this time to mark Mourinho's return, not to disapprove of board decisions
Furaha: Mashabiki Chelsea wakionyesha kumuunga mkono Mourinho
Special
Mourinho
Shepherd: John Terry was rarely threatened by Hull's new signing Yannick Sagbo
John Terry alisumbuliwa mno na mchezaji mpya wa Hull, Yannick Sagbo
New man: Kevin De Bruyne impressed on debut for the Blues
Kifaa kipya: Kevin De Bruyne alivutia akianza kazi The Blues
Bright: Torres looked sharp as he lead the Chelsea line
Torres akipambana
Share:

0 comments:

Post a Comment

KUHUSU MMILIKI WA BLOG HII

My photo
Naitwa faraja Mmasa a.k.a Moa,Mkazi na mzaliwa wa Wilaya ya Gairo Morogoro.KARIBU KATIKA BLOG hii tuelimishane mambo mbalimbali.Inatupasa kuwa na ufahamu wa mambo mbalimbali ili tuweze kuyatawala Mazingira yetu .Kuwa na Mwanasheria au Mhasibu haimanishi unatikiwa kujua au kufuatilia maswala ya uhasibu na sheria tu.Mfano nyumba yako au ndoa yako hutaindesha kwa taaluma uliyonayo.Vile vile huwezi kuendesha ujasiliamali kwa mafanikio kwa shahada yako ya uhandisi.TUNAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA

UJUMBE WA LEO

MIUJIZA MINGI INAYOTOKEA KATIKA MAISHA IPO KATIKA MAWAZO,FIKRA,NA IMANI ALIYONAYO MWANADAMU HUSIKA

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

USIKOSE KIPINDI HOT JIJINI POWER CLUB ,SIBUKA REDIO 94.5 KILA SIKU SAA SABA MPAKA SAA KUMI

GAR AD2

GAR AD2

GARI ADVERT

GARI ADVERT

Castrol

Castrol
Powered by Blogger.